Watu usiku hulala, mimi huketi kalia
Aliyonifanya jana, wala sikutarajia
Ghafula amenikana, moyoni kanisusia
Lipi kwake sijafanya, yote nimemalizia
Na sikufanya khiyana, kwake sikumpimia
Mahaba kila aina, tena mia fil mia
Jee huu ni ungwana, yeye kunikatalia?
Mapenzi hayana mana, kwangu yameniishia
– FaFi
Pole FaFi kwa kulia, haya hayajanza jana
Ndio mwendo wa dunia, binadamu kutendana
Heri penzi kupimia, kwa mja hana amana
Nafsi yako jilindia, hadhari iwe ndo zana
LikeLike